Dollar

42,9413

0.07 %

Euro

50,5553

-0.02 %

Gram Gold

6.157,1600

-1.49 %

Quarter Gold

10.191,0500

-1.43 %

Silver

104,1800

-3.74 %

Mamlaka ya Hali ya Hewa ya Tanzania (TMA) imeonya kuwa mvua kubwa zitanyesha katika mikoa ya 20 ya nchini humo.

Mvua kubwa kunyesha katika mikoa 20 nchini Tanzania

Katika taarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo, TMA iliorodhesha mikoa hiyo ambayo itaathirika na mvua kubwa kuwa Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Kigoma, Katavi, Singida, Dodoma, Rukwa, Songwe na Morogoro.

Mikoa mingine ambayo pia yamewekwa kwenye tahadhari ni Ruvuma, Tanga, Dar es Salaam, Pwani ikiwemo Kisiwa cha Mafia, Lindi, Mtwara, pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba. Mamlaka ya Hali ya Hewa inasema mvua kubwa inaweza kuleta athari mbalimbali.

Miongoni mwa athari zinazotabiriwa ni mafuriko, maporomoko na kutatiza shughuli za uchumi na za kijamii za watu.

Wito umetolewa kwa wakazi katika maeneo yatakayoathirika, hasa wale wanaoishi katika maeneo yenye hatari zaidi, kuchukuwa hatua za kujikinga ili kupunguza athari itakayosababishwa na mvua hizo.

Mamlaka ya Hali ya Hewa pia ilitoa wito kwa umma kufuatilia taarifa watakazokuwa wakitoa mara kwa mara ili waweze kuchukuwa hatua zinazostahiki kuepuka maafa. TMA pia imeonya kuhusu maeneo mengine kuendelea kupata mvua.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#