Jeshi la Marekani latekeleza zuio kwa meli zinazoingia na kutoka bandari za Iran.

Marekani yaanza zuio la baharini dhidi ya Iran

CENTCOM imeanza rasmi kutekeleza zuio dhidi ya usafiri wa baharini unaoingia na kutoka katika bandari za Iran.

Kwa mujibu wa jeshi hilo, hatua hiyo inalenga kudhibiti shughuli za baharini katika Persian Gulf na Gulf of Oman.

CENTCOM imesema kuwa zuio hilo litatekelezwa kwa usawa kwa meli zote bila kujali taifa, likionyesha msimamo wa Marekani katika kuongeza shinikizo kwa Iran.

Hatua hii imeongeza mvutano katika Mashariki ya Kati, huku athari zake zikianza kuonekana katika biashara ya kimataifa na usafirishaji wa nishati.

CHANZO: Newstimehub

#