Dollar

40,9411

0.09 %

Euro

47,9607

0.44 %

Gram Gold

4.383,8900

0.13 %

Quarter Gold

0,0000

%

Silver

0,0000

%

Huku pande zote mbili zikicheza mechi yao ya nne ya CHAN na Nigeria na Sudan zikisubiri katika mbawa, mkutano huu wa kwanza kabisa kati ya Senegal na Congo unaahidi kuchagiza hatima ya kundi hilo.

Kocha wa Senegal atahadharisha juu ya 'mtego wa Kundi D' watakapopambana na DRC kisiwani Zanzibar

‘‘DRC ni mtego kwetu.’’ Maneno mazito kutoka ka kocha wa Senegal Souleymane Diallo anapoiandaa timu yake kukutana na Jamhuri ya Demokrasia ya Congo Jumanne.

Timu zote mbili ni washindi wa zamani huku Senegal wakiwa ndio wanaotetea ubingwa. Japo ndio mara ya kwanza wanakutana katika mashindano haya, wote wanaingia uwanjani wakiwa na mzigo mzito wa kujionyesha ushupavu wao mbele ya mashabiki wa uwanjani na nyumbani.

Kwa Senegal, ushindi ungethibitisha nafasi katika robo fainali. Lakini ukiwaendea Congo, basi itavuruga kabisa hesabu kundini.

Kwa upande wao, Congo wanafika na wamenoa kucha vilivyo. Sare ya 1-1 dhidi ya Sudan siku ya kwanza ya mechi ilidhihirisha uthabiti wao.

Fursa kubadilisha uwiano wa kundi

Walipofungwa mapema kwa bao la Musa Ali Hussein, walipambana na kusawazisha dakika ya 86 kupitia kwa Carly Ekongo aliyemaliza kwa nafasi.

Kocha mkuu Barthélemy Ngatsono, 68, ameona soka la kutosha la shinikizo la juu kujua hii ni fursa ya kubadilisha uwiano wa kundi.

"Baada ya mchezo wa Sudan, tuliondoka pale na mafunzo ya nguvu yetu na udhaifu wetu," Ngatsono alisema.

"Lakini tumefanya mazoezi tukiwa na ufahamu kamili wa nini kiko hatarini dhidi ya Senegal. Hatukuja hapa ili tu kutazama wengine wakinyanyua kombe. Kama ilivyo kwa timu nyingine zote, tuko hapa kwa ajili ya matokeo."

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#