Dollar

43,5337

0.02 %

Euro

51,5353

0.19 %

Gram Gold

6.971,6300

0.89 %

Quarter Gold

12.309,5300

0 %

Silver

122,9800

0.43 %

Rais wa Uturuki Erdogan asema nchi yake inataka kuimarisha ushirikiano na Misri katika nyanja mbalimbali.

Erdogan na Sisi waimarisha ushirikiano kati ya Uturuki na Misri wajadili Gaza na migogoro ya kikanda

Erdogan amesema janga la kibinadamu huko Gaza linaendelea licha ya kuwepo kwa sitisho la mapigano kwa miezi kadhaa. Ameeleza kuwa Uturuki inashirikiana na Misri katika juhudi za kuleta amani Gaza na itaendelea kufanya kazi hiyo kwa karibu.

Akizungumza pamoja na Rais Sisi, Erdogan amesema Misri ni mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa Uturuki barani Afrika. Amebainisha kuwa nchi hizo mbili zinalenga kuongeza biashara kati yao kutoka dola bilioni 8–9 hadi dola bilioni 15 za Marekani, akisisitiza kuwa kuna fursa kubwa za uwekezaji hasa katika sekta za nishati na usafirishaji.

Erdogan pia amesema Uturuki inataka kuimarisha ushirikiano na Misri katika biashara ya baharini, usafiri wa majini, uhuru wa usafiri baharini na usalama wa bahari. Ameongeza kuwa kuimarika kwa uhusiano wa nchi hizo mbili kunaonekana pia katika ongezeko la watalii, na kwamba anatarajia idadi hiyo itaongezeka maradufu katika kipindi kijacho.

Kuhusu masuala ya kikanda, Erdogan amesema Uturuki na Misri zina lengo la pamoja la kulinda umoja na mipaka ya Libya ili kufanikisha utulivu wa kudumu. Ameongeza kuwa Uturuki inataka kwanza kusitishwa kwa mapigano nchini Sudan, kisha kufuatiwa na amani ya kudumu.

Amesema pia kuwa migogoro inayohusisha Iran, ikiwemo suala la nyuklia, inapaswa kutatuliwa kwa njia za kidiplomasia, akionya kuwa uingiliaji wa nje unaweza kuhatarisha usalama wa eneo zima.

Erdogan amesisitiza kuwa Uturuki inaunga mkono mabadiliko makubwa nchini Syria, akisema kuwa umoja wa kisiasa na ulinzi wa mipaka ya Syria utaleta manufaa makubwa kwa eneo lote. Aidha, amekosoa hatua ya Israel kutambua Somaliland kama taifa huru, akisema ni kitendo kinachokiuka mamlaka na umoja wa Somalia.

Kwa upande wake, Rais wa Misri Abdel Fattah el-Sisi amesema Uturuki ni mshirika mkuu wa Misri barani Afrika na kwamba uwekezaji wa Uturuki ni muhimu sana kwa nchi yake. Ameeleza kuwa pande zote mbili zimekubaliana kuongeza biashara hadi kufikia dola bilioni 15.

Sisi pia amesema Uturuki imekuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha sitisho la mapigano Gaza, na kusisitiza umuhimu wa kushirikiana ili kuhakikisha misaada ya kibinadamu inawafikia wahitaji. Amehitimisha kwa kutoa wito wa juhudi za pamoja za kutafuta suluhu za kisiasa za kudumu huku eneo hilo likikabiliwa na misururu ya migogoro.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#