Maafisa wa afya wachunguza chanzo cha maambukizi huku wagonjwa wengine wakifuatiliwa.
Shirika la Afya Duniani limeanzisha uchunguzi wa kina kufuatia mlipuko wa hantavirus uliosababisha vifo vya watu watatu ndani ya meli ya MV Hondius.
Kwa mujibu wa WHO, virusi hivyo kwa kawaida huenezwa kupitia hewa yenye chembechembe kutoka kwenye mkojo au kinyesi cha panya, na vinaweza kusababisha matatizo makubwa ya mfumo wa upumuaji.
Maafisa wa afya wanaendelea kufuatilia hali ya abiria wengine waliokuwa karibu na wagonjwa ili kuzuia kuenea zaidi kwa maambukizi.
CHANZO: Newstimehub