Shirika lasema warsha hizo ni mwanzo wa mpango mpana wa kuinua viwango vya elimu ya kidijitali barani Afrika.

Türkiye Maarif Yapanua Mafunzo ya Sayansi na Teknolojia kwa Walimu wa Afrika

Türkiye Maarif Foundation imesema warsha ya teknolojia iliyofanyika Côte d’Ivoire ni sehemu ya mkakati mpana wa kuboresha elimu ya sayansi na teknolojia katika shule za Afrika.

Rais wa taasisi hiyo, Mahmut Mustafa Özdil, amesema tukio hilo limekusanya Afrika nzima katika jukwaa moja la kujifunza na kubadilishana uzoefu, akieleza kuwa lengo ni kuinua viwango vya kitaaluma na ufundishaji barani humo.

Washiriki walipata mafunzo kuhusu coding ya block-based, gamification, digital design, na matumizi ya vifaa vya kielektroniki kama sensa na circuit katika miradi ya darasani.

CHANZO: Newstimehub

#