Dola bilioni 5 zatoka Abu Dhabi, nyingine bilioni 1 kutoka Uingereza.

Nigeria yapanga kukopa kutoka UAE na Uingereza

Serikali ya Nigeria inapanga kuomba dola bilioni 5 kutoka First Abu Dhabi Bank pamoja na dola bilioni 1 kutoka UK Export Finance.

Fedha hizo zinatarajiwa kuelekezwa katika miradi ya maendeleo, ikiwemo ukarabati wa bandari mbili muhimu zilizoko Lagos.

Serikali inaamini uwekezaji huo utachochea biashara na kuongeza mapato ya taifa.

Mpango huo ni sehemu ya mkakati mpana wa kukuza uchumi na kuboresha miundombinu ya usafirishaji.

CHANZO: Newstimehub

#