Wahamiaji wameanza kufunga biashara zao kwa hofu ya mashambulizi wakati wa maandamano ya kupinga wageni,
Hali ya taharuki imeongezeka nchini Afrika Kusini huku wahamiaji wengi wakiamua kufunga maduka yao kabla ya maandamano yaliyopangwa dhidi ya wageni.
Maandamano hayo yanahusishwa na malalamiko ya baadhi ya wananchi wanaodai kuwa wahamiaji wanachukua nafasi za ajira na kuathiri biashara za wenyeji.
Katika matukio ya nyuma, vikundi vya kupinga wahamiaji vimekuwa vikilazimisha kufungwa kwa maduka ya wageni na hata kufanya uvamizi katika baadhi ya maeneo ya makazi.
Polisi na mamlaka za usalama zimeongeza ulinzi katika maeneo yenye hatari kubwa ili kuzuia vurugu, huku serikali ikisisitiza umuhimu wa kulinda haki za kila mtu bila kujali uraia wake,Wachambuzi wanasema kuwa tatizo la chuki dhidi ya wageni nchini humo linahusishwa na changamoto za kiuchumi kama ukosefu wa ajira na umasikini.
Chanzo:Newstimeshub