Lebanon imesema hatua hiyo ilitokana na "ukiukwaji wa Iram wa kanuni na itifaki za kidiplomasia" kati ya nchi hizo mbili.

Balozi wa Iran nchini Lebanon atimuliwa

Serikali ya Lebanon imetangaza kumfukuza balozi wa Iran nchini humo baada ya kumtangaza rasmi kuwa mtu asiyekaribishwa nchini (persona non grata), hatua inayodhihirisha kuongezeka kwa mvutano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili.

Katika taarifa rasmi, Wizara ya Mambo ya Nje ya Lebanon imesema balozi wa Iran, Mohammad Reza Shibani, anatakiwa kuondoka nchini humo ifikapo tarehe 29 Machi. Hatua hiyo imechukuliwa kutokana na kile ilichoelezwa kuwa ni ukiukwaji wa misingi na taratibu za kidiplomasia unaofanywa na Iran.

Wizara hiyo pia imetangaza kumrejesha balozi wake nchini Iran, Ahmad Sweidan, kwa mashauriano, hatua inayotumika mara nyingi kama ishara ya kutoridhika katika mahusiano ya kidiplomasia.

Chanzo: Newstimehub

#